Nguvu Halisi Iliyopo Ndani Ya Mwanadamu


hello.....
karibu tena kwenye blog yangu, karibu tena kwa ajili ya kujifunza, na baada ya kusoma kama utakuwa na swali..utaliandika kwa kuandika ujumbe wako chini ya hii post...
Barikiwa sana 


Kama vile ambavyo binadamu huitaji chakula ili apate nguvu…na nguvu hiyo huitumia kufanya mambo mengine ya kiroho na kimwili pia…

Vivyo hivyo kwa upande mwingine.. uhai wetu umeshikiriwa na vitu vitatu
Mwili, nafsi na roho

Na ili tuwe hai kamili.. vitu vyote vitatu vinahitaji kulishwa, kutunzwa na kukua, kama vile mwili ukuavyo, mti ukuavyo nk….

Mwili yeye hula chakula cha mwilini, ugali wali nk, nafsi yenyewe huishi kutegemeana na yale tunayowaza na kufikiria ambayo chanzo chake ni milango ya fahamu katika mwili mazingira..…
Roho yenyewe hula chakula cha rohoni…kwa mfano neno la mungu..maombi..nk

Mtu huru yule ambaye mwili wake, nafsi yake na roho yake vianenda sambamba, maana yake ni hivi, mwili wake unatenda kile ambacho nafsi yake unakishuhudia na nafsi yake inatenda kile ambacho roho inakishuhudia….

Maana yake ni nini
Maana yake ni kwamba kile kinachodhihirika nje ya mwili ndicho kilichopo kwenye nafsi na roho yake….
Mtu huyu hatojuta hata siku moja katika kila anachokifanya..maana anachokifanya ni matokeo ya umoja wa mwili, nafsi na roho..

Vitu hivi vitatu visipokwenda sawa inasababisha vitu vifuatavyo..
Woga, hofu kutokujiamini na kukosaa ujasiri, kuwa na maswali mengi yasiyo na majibu..
Ambayo hayo yote husababisha kupungua kwa nguvu ya ndani ya mtu halisi…

Kwahiyo vitu hivi vitatu lazima viwe na mawasiliano hatakama kutakuwa hakuna chakula cha kila mmoja, lazima vyote uvipe taarifa kwamba leo nafsi hautokula.. au mwili hautokula au roho hautokula leo..


Kizazi chetu cha leo kimekuwa kikishindwa kujua namna ya kuviendesha hivi vitu vitatu, na hivyo imepelekea watu wengi kufa kimya kimya…yaani mwili u hai lakini roho imekufa…
Au unakuta mwili upo nafsi imefungwa na roho inalalamika

Na mwingine roho ipo kivyake, mwili kivyake, alkadharika na nafsi kivyake na wengine wameingiwa na roho zingine, ambazo zimesababisha nguvu ya roho halisi kutokuonekana..kwasababu ya kushindwa kuviendesha hivi vitu vitatu…

Mwili hufuata roho kama tu roho atakuwa na nguvu maana yake nini….roho akiwa ameshiba, au kama anachochote kitu, mwili utaladhimika kuifuata roho ambayo mara zote hutoa taarifa ambazo ni sahihi na za kiroho..

Lakini endapo ikitokea roho hana nguvu, mwili hautoweza kusimama peke yake, utaitafuta nafsi kwa ajili ya support,

Na kama tujuavyo nafsi hua na nguvu kutokana na mazingira ya nje ya mwili ambayo huingia ndani ya nafsi kupitia milango ya fahamu…

Na baada ya hapo, mazingira yale hujitengenzea mfumo wa kutawala ambao mfumo huo huipa nafsi nguvu ya kumiliki mfano kutafuta inspirational quotes videos, marafiki ambao utahisi lazima watakuunga mkono,hizo ndo tunaziita nguvu za ziada, kwahiyo katika wakati huo mwili utafata yale ya kwenye nafsi.

Kumbuka roho ni pumzi ya Mungu… maana yake ni mali ya mungu..kwahiyo roho ikishindwa kuendesha mwili asili ya uungu inapungua ndani ya mwanadamu

Kwahiyo nafsi hua inapata nguvu wakati roho ikiwa imekosa nguvu, na baada ya hapo nafsi hujitengenezea makoloni yake kwa kutafuta nguvu kutoka nje ya mwili kupitia milango ya fahamu (nimetoa mifano hapo juu)… ili  mwili uendelee kufanya kazi na mtu aendelee kuishi..

Nafsi Haijalishi mtu ataishi katika mazingira gani, muhimu ni mwili uishi…
Na kwanini nafsi itengeneze mfumo wake wa utawala binafsi… ni ili kuleta balance kwasababu roho wakati hayupo nafsi itatakiwa kubeba nafsi ya roho.. ili mwili uendeshwee…


Sjajua hadi sasa umejifunza nini, lakini katika maisha yako ya kila siku, maamuzi yako yanapaswa kuwa sambamba katika vitengo vyote vitatu ambavyo ni mwili nafsi na roho,,

Kitu ambacho mwili unafanya  na roho inakataa usikipe nafasi.
Kitu unacho kiangalia na kikaondoa Amani ya roho Usikiangalie tena
Maamuzi uliyofanya yakayokuweka mtumwa, achana nayo…

Ingawa Mungu hakuonekana dhahiri katika macho yetu lakini alishaweka mfumo wa utambuzi ndani yetu,,ameweka mfumo wa mawasiliano ndani yetu tayari..

Roho lazima iwe juu ya vyote, tumia muda kuipa roho nguvu juu ya mwili na nafsi.
Mfano tu..
Utakuta maisha ya mchungaji au mwalimu au muhubiri ni tofauti na hayo anayoyahubiri au anayoyafundisha …sababu ni mwili roho na nafsi …au kwa lugha nyingin ni kwamba roho ipo mbali na nafsi na mwili..maana yake mtu huyo ameupa nafasi mwili na nafsi.

Kuwa na uhakika wa maamuzi unayoyafanya lazima kwanza uwe na uhakika wa uwepo wa mawasiliano mazuri kati ya mwili, nafsi na roho,
Lakini cha muhimu Zaidi ni kuongeza nguvu ya roho (kuilisha roho kwa neno la MUNGU), ili nafsi na nguvu za nje ya mwili zisipate nafasi.

Kizazi chetu cha leo kimekuwa kinaishi yale yanayosemwa na si yale yatokayo ndani yao.  Wanaishi wanayoyaona na si yale ambayo ni matokeo ya Imani zao za ndani..

Na hii imesababisha uwepo wa maswali mengi juu ya Imani na matendo yao, hofu nyingi katika kila wanalolitenda.
Hawahitaji ushirika na roho mtakatifu na badala yake wanamuhitaji mwenye ushirika na roho mtakatifu..
Wana Imani lakini bado hawaamini. Wamekuwa watumwa wa Imani zao.


Yesu alisema utaijua kweli na hiyo kweli itakuweka huru, lakini ukija kuangalia watu wengi tunaujua ukweli lakini hatuko huru..
Maana yake nini kuna siri ndani ya iyo kweli ambayo kila mmoja anapaswa kuitambua kwa uwezo wa  roho mtakatifu ili awekwe huru.

Shida kubwa tuliyonayo ni kwamba, hatujui nguvu au uwezo uliopo ndani yetu, na namna ambavyo ukiufanyia kazi vizuri utaweza fika popote unapotaka ili kutimiza ndoto zako.

Your Future is within yourself..
Uwezo wa Kujua usahihi wa yale tunayoyafanya uko pia ndani yetu..
Uwezo wa kujua huyu ndiye, huyu sie pia upo ndani yetu..
Lakini kwasababu hatujui ndomana tunakosea sana kutafuta nguvu nyingine nje na kusahau iliyopo ndani yetu..

Tafuta kujua nguvu na uwezo uliopo ndani yako kila siku..
maana hata sasa hakuna aliyejua uwezo wote alionao ndani yake, lakini tunakavyovijua ndivyo hivyo tunafanyia kazi.

Jifunze namna ya kuendesha hisia zako, mawazo, kuifunza akili yako kwa kuipa vitu unavyoona unavyovihitaji au utakavyovihitaji..
Kuwa msikilizaji sana kuliko kuwa muongeaji..
Fikiri sana kabla ya kutenda.
Focus yourself on building strong foundation of your own faith, to the point that you can stand and defend it, to the point that no one will shake you.


Itaendelea…



Comments

  1. Asante Sana Kwamafundisho yako manzuri
    "Shida kubwa tuliyonayo ni kwamba, hatujui nguvu au uwezo uliopo ndani yetu, na namna ambavyo ukiufanyia kazi vizuri utaweza fika popote unapotaka ili kutimiza ndoto zako." Angel Fabian quotes

    ReplyDelete

Post a Comment

Dont miss these ones

Where our HoPe IS....??

LET ME KNOW YOUR MISSION IN MY LIFE

Moyo wa Mtu ni Kama Kichaka