Nguvu Halisi Iliyopo Ndani Ya Mwanadamu


Hello.....
Karibu tena kwenye blog yangu, karibu tena kwa ajili ya kujifunza, na baada ya kusoma kama utakuwa na swali..utaliandika kwa kuandika ujumbe wako chini ya hii post...
Barikiwa sana 

Kama vile ambavyo binadamu huitaji chakula ili apate nguvu…na nguvu hiyo huitumia kufanya mambo mengine ya kiroho na kimwili pia…

Vivyo hivyo kwa upande mwingine.. uhai wetu umeshikiriwa na vitu vitatu
Mwili, Nafsi na Roho

Na ili tuwe hai kamili.. vitu vyote vitatu vinahitaji kulishwa, kutunzwa na kukua, kama vile mwili ukuavyo, mti ukuavyo nk….

Mwili yeye hula chakula cha mwilini, ugali wali nk, nafsi yenyewe huishi kutegemeana na yale tunayowaza na kufikiria ambayo chanzo chake ni milango ya fahamu katika mwili mazingira..…
Roho yenyewe hula chakula cha rohoni…kwa mfano neno la Mungu..maombi..nk

Mtu huru yule ambaye mwili wake, nafsi yake na roho yake vinaenda sambamba, maana yake ni hivi, mwili wake unatenda kile ambacho nafsi yake unakishuhudia na nafsi yake inatenda kile ambacho roho inakishuhudia….

Maana yake ni nini........
Maana yake ni kwamba kile kinachodhihirika nje ya mwili ndicho kilichopo kwenye nafsi na roho yake….
Mtu huyu hatojuta hata siku moja katika kila anachokifanya..maana anachokifanya ni matokeo ya umoja wa mwili, nafsi na roho..

Vitu hivi vitatu visipokwenda sawa inasababisha vitu vifuatavyo..
Woga, hofu kutokujiamini na kukosaa ujasiri, kuwa na maswali mengi yasiyo na majibu..

Tusome maandiko ya Mtume paulo, Warumi 7:15-25 namna alivyopitia hali ya mashindano kati ya mwili nafsi na roho yake.

''Tunafahamu kwamba sheria ni ya kiroho. Lakini mimi si wa kiroho; mimi nimeuzwa utumwani, ni mtumwa wa dhambi. 15 Sielewi nitendalo: kwa maana lile ninalotaka kulifanya, sifanyi; badala yake, ninafanya lile ambalo nachukia kulifanya. 16 Kwa hiyo kama ninafanya lile nisilopenda kufanya, hii ina maana kwamba nakubali kuwa sheria ni njema. 17 Basi, kwa kweli si mimi hasa nitendaye lile nisilolipenda bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu. 18 Kwa maana ninafahamu kwamba hakuna wema wo wote ndani yangu mimi, yaani katika mwili wangu wa asili. Ingawa nina nia ya kutenda lililo jema, lakini ninashindwa kulitenda. 19 Sitendi lile jema nipendalo bali lile ovu nisilopenda, ndilo nitendalo. 20 Basi kama ninafanya lile nisilopenda kufanya, si mimi tena nifanyaye hivyo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu.
21 Kwa hiyo imekuwa kama ni sheria: kila ninapotaka kufanya jambo jema, jambo ovu hujitokeza. 22 Kwa maana ndani yangu ninaifurahia sheria ya Mungu. 23 Lakini ninaona kuna sheria nyin gine mwilini mwangu inayopingana na ile sheria ninayoikubali akilini mwangu. Sheria hii inanifanya kuwa mateka wa sheria ya dhambi ambayo inafanya kazi mwilini mwangu.
24 Ole wangu, mimi mnyonge! Ni nani atakayeniokoa na huu mwili wa kifo? 25 Ninamshukuru Mungu kwa ajili ya Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa hiyo basi, mimi kwa moyo wangu, ninaitumikia sheria ya Mungu, lakini kwa mwili wangu wa asili ninaitumikia sheria ya dhambi.

Hivyo hapo tunajifunza, Asili ya mwili ni dhambi na uovu, na namna pekee ya kuutiisha mwili ni, kuilisha nafsi  kile unachotaka kitokee na roho ambayo ina asili ya uungu ili viweze kuwa na nguvu ya kuuongoza mwili.

Ambayo hayo yote husababisha kupungua kwa nguvu ya ndani ya mtu halisi…

Kwahiyo vitu hivi vitatu lazima viwe na mawasiliano hatakama kutakuwa hakuna chakula cha kila mmoja, lazima vyote uvipe taarifa kwamba leo nafsi hautokula.. au mwili hautokula au roho hautokula leo..

Kizazi chetu cha leo kimekuwa kikishindwa kujua namna ya kuviendesha hivi vitu vitatu, na hivyo imepelekea watu wengi kufa kimya kimya…yaani mwili u hai lakini roho imekufa, au unakuta mwili upo nafsi imefungwa na roho inalalamika (unakuwa mateka)

Na mwingine roho ipo kivyake, mwili kivyake, alkadharika na nafsi kivyake na wengine wameingiwa na roho zingine, ambazo zimesababisha nguvu ya roho halisi kutokuonekana..kwasababu ya kushindwa kuviendesha hivi vitu vitatu kwa maana nyingine ni kuwa mateka kama mtume Paulo anavyosema. …

Mwili hufuata roho kama tu roho atakuwa na nguvu maana yake nini….roho akiwa ameshiba, au kama anachochote kitu, mwili utaladhimika kuifuata roho ambayo mara zote hutoa taarifa ambazo ni sahihi na za kiroho..

Lakini endapo ikitokea roho hana nguvu, mwili hautoweza kusimama peke yake, utaitafuta nafsi kwa ajili ya support,

Na kama tujuavyo nafsi hua na nguvu kutokana na mazingira ya nje ya mwili ambayo huingia ndani ya nafsi kupitia milango ya fahamu…

Na baada ya hapo, mazingira yale hujitengenzea mfumo wa kutawala ambao mfumo huo huipa nafsi nguvu ya kumiliki mfano kutafuta inspirational quotes videos, marafiki ambao utahisi lazima watakuunga mkono,hizo ndo tunaziita nguvu za ziada, kwahiyo katika wakati huo mwili utafata yale ya kwenye nafsi.

Kumbuka roho ni pumzi ya Mungu… maana yake ni mali ya Mungu..kwahiyo roho ikishindwa kuendesha mwili asili ya uungu inapungua ndani ya mwanadamu

Kwahiyo nafsi hua inapata nguvu wakati roho ikiwa imekosa nguvu, na baada ya hapo nafsi hujitengenezea makoloni yake kwa kutafuta nguvu kutoka nje ya mwili kupitia milango ya fahamu (nimetoa mifano hapo juu)… ili  mwili uendelee kufanya kazi na mtu aendelee kuishi..

Nafsi haijali mtu ataishi katika mazingira gani, muhimu ni mwili uishi…
Na kwanini nafsi itengeneze mfumo wake wa utawala binafsi… ni ili kuleta balance kwasababu roho wakati haina nguvu nafsi itatakiwa kubeba nafsi ya roho.. ili mwili uendeshwee…

Sijajua hadi sasa umejifunza nini, lakini katika maisha yako ya kila siku, maamuzi yako yanapaswa kuwa sambamba katika vitengo vyote vitatu ambavyo ni mwili nafsi na roho,,

Kitu ambacho mwili unafanya  na roho inakataa usikipe nafasi.
Kitu unacho kiangalia na kikaondoa Amani ya roho Usikiangalie tena
Maamuzi uliyofanya yakayokuweka mtumwa, achana nayo…

Ingawa Mungu hakuonekana dhahiri katika macho yetu lakini alishaweka mfumo wa utambuzi ndani yetu,,ameweka mfumo wa mawasiliano ndani yetu tayari..

Roho lazima iwe juu ya vyote, tumia muda kuipa roho nguvu juu ya mwili na nafsi.
Mfano tu..
Utakuta maisha ya mchungaji au mwalimu au muhubiri ni tofauti na hayo anayoyahubiri au anayoyafundisha …sababu ni mwili roho na nafsi …au kwa lugha nyingin ni kwamba roho ipo mbali na nafsi na mwili..maana yake mtu huyo ameupa nafasi mwili na nafsi.

Kuwa na uhakika wa maamuzi unayoyafanya lazima kwanza uwe na uhakika wa uwepo wa mawasiliano mazuri kati ya mwili, nafsi na roho,
Lakini cha muhimu Zaidi ni kuongeza nguvu ya roho (kuilisha roho kwa neno la MUNGU), ili nafsi na nguvu za nje ya mwili zisipate nafasi.

Kizazi chetu cha leo kimekuwa kinaishi yale yanayosemwa na si yale yatokayo ndani yao.  Wanaishi wanayoyaona na si yale ambayo ni matokeo ya Imani zao za ndani..

Na hii imesababisha uwepo wa maswali mengi juu ya Imani na matendo yao, hofu nyingi katika kila wanalolitenda.
Hawahitaji ushirika na roho mtakatifu na badala yake wanamuhitaji mwenye ushirika na roho mtakatifu..
Wana Imani lakini bado hawaamini. Wamekuwa watumwa wa Imani zao.


Yesu alisema utaijua kweli na hiyo kweli itakuweka huru, lakini ukija kuangalia watu wengi tunaujua ukweli lakini hatuko huru..
Maana yake nini kuna siri ndani ya iyo kweli ambayo kila mmoja anapaswa kuitambua kwa uwezo wa  roho mtakatifu ili awekwe huru.

Shida kubwa tuliyonayo ni kwamba, hatujui nguvu au uwezo uliopo ndani yetu, na namna ambavyo ukiufanyia kazi vizuri utaweza fika popote unapotaka ili kutimiza ndoto zako.

Your Future is within yourself..
Uwezo wa Kujua usahihi wa yale tunayoyafanya uko pia ndani yetu..
Uwezo wa kujua huyu ndiye, huyu sie pia upo ndani yetu..
Lakini kwasababu hatujui ndomana tunakosea sana kutafuta nguvu nyingine nje na kusahau iliyopo ndani yetu..

Tafuta kujua nguvu na uwezo uliopo ndani yako kila siku..
maana hata sasa hakuna aliyejua uwezo wote alionao ndani yake, lakini tunakavyovijua ndivyo hivyo tunafanyia kazi.

Jifunze namna ya kuendesha hisia zako, mawazo, kuifunza akili yako kwa kuipa vitu unavyoona unavyovihitaji au utakavyovihitaji..
Kuwa msikilizaji sana kuliko kuwa muongeaji..
Fikiri sana kabla ya kutenda.
Focus yourself on building strong foundation of your own faith, to the point that you can stand and defend it, to the point that no one will shake you.


Itaendelea…



Comments

  1. Asante Sana Kwamafundisho yako manzuri
    "Shida kubwa tuliyonayo ni kwamba, hatujui nguvu au uwezo uliopo ndani yetu, na namna ambavyo ukiufanyia kazi vizuri utaweza fika popote unapotaka ili kutimiza ndoto zako." Angel Fabian quotes

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular Posts